BlinkBlog

Wakati wa Mungu ndio Sahihi, asema Joyce Omondi baada ya fununu kwamba ni mjamzito

- Mwanamuziki wa nyimbo za injili Joce Omondi amevunja kimya chake kufuatia madai kwamba ana ujauzito

- Joyce na mtangazaji Wahiga Mwaura walifunga pingu za maisha mwaka wa 2015 kwenye sherehe ya kukata na shoka

- Ndoa yao imekuwa ya kutamanika na wengi kwenye mitandao ya kijamii ila bado hawajajaliwa watoto

Mtangazaji na mwanamuziki maarufu wa nyimbo za injili Joyce Omondi amewajibu mashabiki wake ambao wamekuwa wakidai kwamba ana ujauzito.

Habari Nyingine: Picha Maridadi za Binti Mrembo wa Rais Uhuru, Ngina Kenyatta

Habari Nyingine: Ruth Matete Achapisha Ujumbe wa Huzuni Akiadhimisha Kifo cha Mumewe

Madai ya yeye kuwa mjamzito yaliibuka baada ya kuvalia rinda lilionekana kuwa la uzazi, yaani maternity dress.

Joyce na mumewe mtangazji wa runinga ya Citizen Wahiga Mwaura walifanya harusi ya kufana Disemba 2015 lakini bado hawajajaliwa mtoto.

Akiyajibu madai hayo, Joyce alikuwa na haya ya kusema," Kwa hivyo muundo wa rinda hili umefanya watu waanze kufikiria visivyo, hata hivyo wakati wa Mungu ndio sahihi lakini asanteni kwa upendo wenu," Aliandika Joyce.

Baadhi ya mashabiki wake walimtia moyo wakimweleza kwamba wanamuombea sana abarikiwe na mtoto.

" Kila mtu anakuombea, jinsi ulivyoonekana kwenye picha hiyo ilikuwa wazi kwamba una ujauzito, hata hivyo hebu na Mungu akutendee na abariki tumbo lako la uzazi. Unapendeza sana," Gacerikamum aliandika.

Shabiki wake mwingine aliyetambulika kama Kibet Kiptoo aliandika," Hongera Joyce kwa kazi nzuri, ni vema haujamfeli ' BoyChild'.

Habari Nyingine: Rais Suluhu Avua Barakoa Pindi Alipotua Tanzania Kutoka Ziarani Uganda

Wahiga pamoja na mkewe wamekuwa wakionyesha mapenzi yao hadharani na kufanya wawe tamanio kwa wengi hasa wanadada ambao bado wanasaka penzi.

Mwaka jana Wahiga alimtumia Joyce ujumbe mtamu siku yake ya kuzaliwa.

"Heri njema malkia wa roho yangu, furahia siku ya leo kwa sababu ni muhumu sana kwetu sisi. Hebu na uhisi upendo kila dakika ya mwaka huu," Aliandika Wahiga.

Read: ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari zaidi kutoka hapa TUKO.co.ke

Subscribe to watch new videos

Chanzo: TUKO.co.ke

ncG1vNJzZmijmajEorTIpaBnrKWgvG%2BvzmeinmdkZYV1gphmrpqjkam2bsPAZqSuppeqeq%2BwyKhkrJmYnrWqecCsnKaZXZ%2B8uq%2FEZqamp56Ztm6uwJqbmmWplnqnwc2upa5lm6yurq7AZqWiZZ2frq7GyK2mZ6Ckork%3D

Aldo Pusey

Update: 2024-07-21